
Kwa ufupi
- Yanga ndiyo inaongoza Ligi Kuu kwa sasa ikiwa na pointi 29, ikifuatiwa na Azam na Mbeya City zenye pointi 28 kila moja.
- Mkwasa na Pondamali waliwahi kuwa wachezaji wa Yanga na wamepewa jukumu la kuwa wasaidizi, huku uongozi wa klabu hiyo ukiendelea na harakati za kutafuta kocha mkuu kutoka barani Ulaya, atakayekuja kurithi mikoba ya Kocha Ernest Brandts na hadi sasa ni zaidi ya makocha 45 wameomba kuchukua jukumu hilo.
Mkwasa aliyekuwa kocha mkuu wa Ruvu Shooting amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha Yanga akichukua jukumu la kuwa kocha msaidizi.
Hata hivyo, kwa sasa Mkwasa atatekeleza majukumu
yake akiwa kaimu kocha mkuu wa Yanga akirithi nafasi iliyoachwa wazi na
Ernest Brandts alifungashiwa virago hivi karibuni sambamba na benchi
zima la ufundi la timu hiyo.
Akizungumza baada ya mazoezi ya kikosi chake jana
asubuhi Mkwasa alisema, hatakuwa tayari kutoa nafasi kwa mchezaji wake
yeyote kumtawala kwani endapo ataruhusu hali hiyo timu itakosa nidhamu.
“Kimsingi Yanga ina wachezaji wazuri ingawa wanahitaji stamina ya kutosha na ndicho kitu ambacho nimeanza nacho leo na baada ya hapo tutaendelea na vitu vingine.
“Isipokuwa nasisitiza nidhamu kwangu ndiyo kila
kitu ili timu iweze kufanya vizuri na nitatilia mkazo hilo, mchezaji
ambaye hatakuwa tayari kufuata taratibu zilizowekwa ajue hana nafasi
kwangu,” alisema Mkwasa.
Katika mazoezi hayo yaliyodumu kwa saa 2:15,
mwandishi wa gazeti hili aliwashuhudia wachezaji wa Yanga wakifanya
mazoezi ya kukimbia, viungo na namna ya kukokota mpira na kupiga
mashuti.
Kwa upande wake, kocha mpya wa makipa wa Yanga,
Juma Pondamali ambaye kama ilivyo kwa Mkwasa alianza kibarua chake jana
alisema:”Nilikuwa na progamu 12 za mazoezi, lakini makipa wangu
wamenilalamikia kwamba uwanja ni mbovu hivyo nimelazimika kuishia
programu nane.
“Pamoja na hayo nimewaambia hivi ndivyo viwanja
vyetu wanatakiwa wakubaliane na hali halisi maana sitaweza kuharibu
programu zangu kwa sababu ya uwanja.”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni