
Kwa mujibu wa Global Publishers, msanii wa filamu na muziki Snura Mushi amesema kuwa Wema ndiye aliyemlipia gharama za studio za kurekodi wimbo wake wa kwanza ‘Shogaake Mama’, hivyo amemshukuru kwa kuwa mchango mkubwa katika muziki wake.

“Namshukuru Wema, kwani alihusika sana kwenye wimbo wangu wa kwanza wa ‘Shogaake Mama’ kwani fedha yake ndiyo ilitumika kurekodi wimbo huo pia aliingiza sauti yake kwenye wimbo huo, alinibunia vazi la shoo yangu ya kwanza ambalo ninaliendeleza mpaka sasa,” alisema Snura.
Snura alifanikiwa kuingia katika chart mbalimbali za muziki Tanzania mwaka huu kwa single yake ‘Majanga’ iliyopata mafanikio makubwa yaliyomuwezesha kupata show nyingi. Single hiyo ilifuatiwa na single nyingine ‘Nimevurugwa’ ambayo hata hivyo haijafanikiwa kufikia mafanikio ya ‘Majanga’.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni